The House of Favourite Newspapers

Utajiri wa Mark Zuckerberg Waporomoka

0
Utajiri wa Mwanzilishi wa Facebook, Mark Zuckerberg umeanguka kwa wastani wa USD bilioni 5.9 hadi USD bilioni 7 (takribani Tsh trilioni 13) wakati mitandao ya Facebook, Instagram na Facebook ilipata tatizo la kimtandao na kumshusha hadi namba 6 kwenye orodha ya matajiri Duniani akiwa na utajiri wa USD bilioni 116. 8.

Kampuni ya Facebook imethibitisha kwamba Mitandao yake ya Facebook, Instagram na WhatsApp imerejea hewani baada ya kupata tatizo na kufanya baadhi ya watumiaji kushindwa kufanya chochote kwenye Account zao, kwenye taarifa yao wameomba radhi Wateja wote Duniani.

 

Kampuni ya Faceebok imesema kilichosababisha tatizo la kimtandao lililopeleka baadhi ya watumiaji wa Instagram, WhatsApp na Faceebok kushindwa kufanya chochote kwenye Account zao ni kufeli kwa mabadiliko ya mfumo, wafanyakazi wa Faceebok wanasema tatizo ni la ndani na sio udukuzi.

Leave A Reply