The House of Favourite Newspapers

UTASHANGAA: Ajifungua Mapacha 4 Kwa Mara Ya Pili Mfululizo! – VIDEO

Mwanamama Jenifa John, Mkazi wa Kigoma, Mapema  jana amejifungua watoto wanne wote wakiwa hai katika Hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou Toure.

Jenifa ameeleza kuwa hiyo sio mara yake ya kwanza kujifungua watoto wanne kwani aliwahi mara ya kwanza alijifungua watoto wanne akiwa na mimba ya miezi sita lakini watoto hao wote walifariki na hii ni mara yake ya pili kujifungua idadi hiyo ya watoto kwa uzao mmoja.

Aidha Jenifa ameiomba Serikali kumsaidia kulea watoto wake ili watoto hao waweze kupata huduma zinazostahiki kwani Mungu amemsaidia kujifungua watoto wote wazima.

Comments are closed.