The House of Favourite Newspapers

Uwatu kwa Kuondoa Chunusi

Uwatu

LEO kwenye safu yetu ya tiba kwa chakula tutaona jinsi Uwatu unavyoweza kukuondolea chunusi kabisa na ukasahau tatizo hilo.

 

JINSI YA KUUANDAA

Saga uwatu ili upate unga wake Baada ya hapo uchukue unga huo uweke kwenye kibakuli changanya na asali kiasi na maji masafi kiasi. Ukimaliza paka usoni kisha fanyia masaji uso wako.

 

Masaji hii itakusaidia unga wa uwatu kuingia ndani ya ngozi na kutibu kabisa tatizo hilo la chunusi pamoja na vipele vidogovidogo.

Lakini ili kuwa na ngozi nzuri zaidi changanya na sukari pia itakusaidia.

Comments are closed.