VIDEO: HARMONIZE Alamba Dili la Maana Bongo
Mapema leo Jumatano, Januari 15, 2020, Msanii Rajab Abdul maarufu kama Harmonize (Kondeboy) ameingia makubaliano na kampuni ya Sayona kuwa balozi wa kinywaji cha Sayona Twist Tanzania.
Sayona wamemtambulisha Harmonize wakati wa Mkutano uliofanyika mbele ya waandishi wa habari katika Hoteli ya White Sand jijini Dar es Salaam.
Harmonize amesema makubaliano mapya na kampuni ya #Sayona ndio sababu ya mgahawa wa ‘Konde Boy’ uliopo katika gari kutoonekana mtaani kwasasa.