The House of Favourite Newspapers

Wadau Walivyoipongeza NIC Goba Hills Marathon

0
Mbio zikianza.

Wadau mbalimbali walioshiriki mbio za NIC Goba Hills Marathon wamezipongeza mbio zilizokuwa na lengo la kuimarisha afya zao pamoja na kusaidia kuchangia afya ya mama wajamzito na watoto.

Mbio hizo ziliwashirikisha wadau kutoka taasisi mbalimbali zifanyika Jumamosi iliyopita ambapo miongoni mwa walioshiriki ni Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (ZCO) Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Camilius Wambura aliyeshiki mbio za kilomita 10, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Building Works LTD, Mohamed Noray aliyeshiki mbio za kilomita 5 na wengineo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Building Works LTD, Mohamed Noray akimaliza mbio za kilomita 5.

Mbio hizo zilianzia Shule ya Sekondari ya Goba zikiwa na wakimbiaji wa viwango tofauti ambapo mbio ndefu zaidi ilikuwa ni kilomita 42 ambapo pia kulikuwa na mbio za kilomita 21 kilomita 10 na kilomita 5.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Building Works LTD, Mohamed Noray akionesha medali aliyokabidhiwa baada ya kumaliza mbio hizo.

Baada ya kumaliza mbio hizo Noray aliwashukuru waandaaji wa mbio hizo pamoja na wadhamini wakuu Shirika la Bima la Taifa (NIC) ambazo zimewasaidia kuimarisha afya zao pamoja na kuchangia fedha kwaajili ya afya ya mama wajawazito na watoto.

Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (ZCO), Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Camilius Wambura akizungumza na wanahabari baada ya kumaliza mbio za kilomita 10.

SACP Camilius Wambura naye aliwasifu waandaji na waliojitokeza kwenye mbio hizo kwa umoja na amani waliouonesha na kujenga afya zao.

Mohamed Noray akizungumza na wanahabari (hawapo pichani).

“Michezo kama hii ni muhimu sana katika jamii haswa kipindi hiki cha janga la Covid-19 kwani kwa zoezi kama hili ni zaidi ya kujifusha”. Alimaliza kusema SACP Wambura.         HABARI/PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL

Leave A Reply