Wadhamini Waomba Lissu Akamatwe – Video
WADHAMINI wa aliyekuwa mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, wamewasilisha maombi mahakamani kutaka itoe kibali cha Lissu kukamatwa baada ya kushindwa kumshawishi arejee nchini.
Lissu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anakabiliwa na kesi ya uchochezi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu huku mahakama hiyo ikitaka wadhamini wahakikishe anarejea nchini.