The House of Favourite Newspapers

Wamiliki wa Malori Wawaweka Mtu Kati, Tanrod, TRA, LATRA, EWURA

0
Mwenyekiti wa TAMSTOA, Chuki Shabani akizungumza kwenye mkutano huo.

 

 

CHAMA cha wamiliki wa malori wadogo na wakati nchini TAMSTOA kimeziweka mtu taasisi za serikali wanazofanya nazo kazi na kuwapa changamoto wakiwemo Mamlaka ya Mapato nchini TRA, LATRA, Tanrod, EWURA na Jeshi la Polisi.

Mwanachama wa TAMSTOA, Mgendela Gama akieleza changamoto wanazokumbana nazo kwenye uendeshaji wa shughuli hiyo.

 

 

 

TAMSTOA iliwaweka kikaangoni wadau wake hao kwenye mkutano wao mkuu wa pili uliofanyika Hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro Hotel jijini Dar Alhamisi iliyopita.

Baadhi ya viongozi wa TAMSTOA na Taasisi za Serikali zilizoalikwa wakiwa meza kuu kusikiliza changamoto za wanachama.

 

 

Katika mkutano huo ambao wamiliki hao wa malori waliwaalika wadau mbalimbali waliwaelezea changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika utendaji wao wa kazi.

 

Akizungumzia changamoto zinazowakabili kwenye uendeshaji wa shughuli zao Mwenyekiti cha chama hicho Chuki Shabani alizitaja baadhi yake kuwa ni upandaji bei za mafuta kiholela, magari yao kukamatwa bila sababu za msingi, kutozwa kodi nyingi tofauti na wenzao wa nchi jirani jambo linalosababisha baadhi ya Watanzania kuyasajili malori yao nchi hizo ili kukimbia kodi kubwa zinazotozwa hapa nchini.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya TAMSTOA na Msemaji wa chama hicho Mark Gama akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) baada ya mkutano huo.

 

 

 

Akizungumza na wanahabari msemaji wa Mjumbe Wa Kamati Kuu ya TAMSTOA na Msemaji wa chama hicho, Mark Gama ameiomba serikali kuwapunguzia changamoto hizo ili waendelee kufanya shughuli zao kiufanisi na kuweza kulipa mapato ya taifa.

Sehemu ya wanachama wakisikiliza kinachoendelea kwenye mkutano huo.

 

 

 

Gama pia ametumia nafasi hiyo kiumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuingilia wana popatwa na matatizo kaka hivi karibuni alivyowasaidia katika sakata la madereva wao waliobeba magogo walivyokamatwa nchini Zambia.

HABARI/PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL

Leave A Reply