WASHINDI watatu wa droo ya tano ya shindano la ‘Shinda Nyumba’ leo wameondoka na zawadi zao katika ofisi za Global Publishers zlizoko Mwenge-Bamaga jijii Dar es Salaam.
Washindi hao ni Ummy Ally kutoka Dodoma ambaye aliwakilishwa na ndugu yake, Judah Rasul, aliyemchukulia zawadi ya vyombo vya nyumbani (dinner set); mwengine ni Festo Masigasi kutoka Bunju ambaye alishinda simu ya kisasa (smart phone) na David Shagalawa ambaye alishinda televisheni ya ukutani (flat screen).
Wakizungumza na gazeti la Amani kwa nyakati tofauti, washindi hao waliishukuru kampuni yaGlobal Publishers kwa zawadi hizo huku wakitoa wito kwa watu wengine kushiriki katika shindano hilo ambalo ni maarufu nchini.
“Naishukuru Global Publishers kwa zawadi hii, hakika nilidhani mambo haya ni ya kupeana lakini ukweli ni kwamba hakuna mazingira ya kupeana, kila mtu anashinda kutokana na bahati yake,” alisema Restuta Shangalawa aliyepokea zawadi kwa niaba ya David Shangalawa, mshindi kutoka Kigoma.
Ofisa Masoko wa Global Publishers, Yohana Mkanda, aliitoa wito kwa wasomaji kuendela kujaza kuponi zilizoko magazetini na kushiriki katika shindano la Shinda Nyumba ambalo linabadilisha maisha ya watu wengi nchini.
“Watu waendelee kujaza kuponi ili wajisogeze kwenye nafasi kubwa ya ushindi kwani shindano hili limebadilisha maisha ya watu wengi sana. Kwa hiyo watu wachangamkie fursa hii,” alisisitiza ofisa huyo.
Na Ally Katalambula | GPL