Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi amethibitisha kupokea taarifa za ajali hiyi na kusema Watanzania hao walikwenda Uganda kwa ajili ya shughuli ya harusi lakini hana taarifa walikwenda sehemu gani nchini humo. Amesema wanaendelea kufanya mawasiliano na mamlaka za Uganda kujua undani wa ajali hiyo.
“Ni kweli tumefuatilia basi hilo na kubaini kwamba liliondoka hapa nchini Septemba 15 kwenda Uganda kwenye shughuli ya harusi. Mengine siwezi kusema zaidi mpaka tutakapofanya mawasiliano na mamlaka za Uganda,” amesema Ollomi.