The House of Favourite Newspapers

Watuhumiwa 267 Wakamatwa na Polisi Pasaka

0
Kamishna wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Simon Sirro, akizungumza na wanahabari.

JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limesema limewakamata watuhumiwa 267 wa makosa mbalimbali ya uhalifu  wakiwemo wa madawa ya kulevya  kipindi cha kuelekea sikukuu ya Pasaka kati ya Aprili 13 na 17 mwaka huu.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Kanda Maalum Dar es Saalam, Simon Sirro,  amesema kukamatwa kwa watuhumiwa hao kunatokana na juhudi kubwa za wananchi kutoa taarifa kwa jeshi hilo na kusababisha kufaniksha kunaswa kwa watuhumiwa hao.

Mkutano ukiendelea.

Ameleza kuwa baadhi ya watuhumiwa wamekamatwa kutokana na makosa ya unyang’anyi na  kutumia silaha, nguvu, utapeli, wizi kutoka maungoni, kucheza kamari, kuuza pombe haramu ya gongo na kupatikana na bangi.

Sirro akionyesha baadhi ya silaha zilizokamatwa katika oparesheni hiyo.

Aliongeza kwamba katika operesheni hiyo pia jumla ya kete 366 za dawa za kulevya zimekamatwa huku puli zikiwa 150, misokoto ya bangi 51  na pombe haramu ya gongo lita 200.

Baadhi ya vitu vingine vilivyokamatwa katika oparesheni hiyo.
Sirro akisikiliza kwa makini maswali ya wanahabari.

Amewaomba  raia wema kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kurahisisha kukamatwa kwa wahalifu. Watuhumiwa wote waliokamatwa bado wanaendelea kuhojiwa kulingana na makosa yao na pindi upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi.

Na Denis Mtima/GPL

Leave A Reply