The House of Favourite Newspapers

Bakwata Kujadili Mmomonyoko wa Maadili Nchini

0
Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Bakwata na msemaji wa Mufti Mkuu wa Tanzania (mwenye kofia), Khamis Mataka, akizungumza na wanahabari. Pembeni mwake ni Mkurugenzi wa Habari makao makuu ya Bakwata, Horera.

BARAZA Kuu la Waislam Tanzania (Bakwata) linatarajia kufanya mkutano utakaojadili hali ya mmomonyoko wa maadili unavyoathiri jamii nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Bakwata na  msemaji wa Mufti Mkuu wa Tanzania, Khamis Mataka, alisema mkutano huo utafanyika Aprili 24 mwaka huu katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais John Magufuli.

Mkutano na wanahabari ukiendelea.

Mkutano huo pia unatarajiwa kuwakutanisha mabalozi kutoka nchi mbalimbali, masheikh wa mikoa mbalimbali na watu wengine.

Na Denis Mtima/GPL

Leave A Reply