Waziri wa TAMISEMI, Seleman Jafo leo Feb 7, 2020 amepiga marufuku wakuu wa mikoa, wilaya, makatibu tawala wa mikoa na wilaya pamoja na wakurugenzi wa halmashauri kutoka nje ya vituo vya kazi kwenda kuhudhuria mikutano, semina na warsha mbalimbali na amefuta vibali vyote vilivyotolewa kwa ajili ya safari hizo.