Waziri Kairuki Akutana Na Waongoza Watalii, Asikiliza Kero Zao – Video
Waziri wa Maliasili na Utalii, Angellah Kairuki (Mb) amefanya kikao na Waongoza Watalii kwa lengo la kusikiliza changamoto zao, maoni na ushauri wa kuiboresha Sekta ya Utalii nchini kilichofanyika katika Jengo la Ngorongoro jijini Arusha.
Kikao hicho kimehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi pamoja na Watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii na Taasisi zake.