Waziri Shonza Awageukia Wabunifu wa Mavazi
Naibu Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza amewataka wabunifu mavazi nchini kuungana na Mbunifu mwenzao, Ally Rehmtullah aliyewapa fursa ya kutumia ofisi yake iliyopo Barabara ya Chole, Masaki Dar es Salaam.
Shonza amempongeza Rehmtullah kwa kujitolea ofisi hiyo ambayo itasaidia kuwaunganisha wabunifu hao kubadilishana ujuzi na kuboresha vipaji vyao.
Aliongeza kwa kusema umoja huo utawapa mafanikio makubwa na kuweza kulipa kodi kwa serikali kama alivyofikia mwenzao Rehmtullah.
HABARI: NEEMA ADRIAN | PICHA: RICHARD BUKOS/GPL