Waziri Ummy “Tunahitaji Samia Suluhu Bus Stendi Mkuranga- Video
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi amesema Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga inahitajika Stendi kubwa kama ile ya Magufuli iliyopo Mbezi Louis Dar es salaam, ameyasema hayo wakati alipofika halmashauri hiyo kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo.
Waziri Ummy amesema kutokana na kuwepo na uhitaji wa stendi hiyo atahakikisha fedha zinapatina sambamba na kutaka barabara ya mwendokasi kufika mpaka mwandege wilayani humo.
Awali mbunge wa jimbo hilo la Mkuranga ambaye pia ni naibu waziri wa Mifugo na uvuvi amesema eneo tayari lipo na ikipatikana stendi hiyo itasaidia wananchi hao kiuchumi.