The House of Favourite Newspapers

Wellu Akiri Kubadili Dini Mazima

MWANAMAMA sexy kunako Bongo Movies, Wellu Sengo amekiri kubadili dini mazima kutoka Ukristo kwenda Uislam huku akisisitiza kuwa hawezi kuzuia watu kuzungumza wanachojisikia.

Katika mahojiano maalum na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Wellu ambaye ni mzazi mwenza wa komediani Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ alisema ameamua kurudi kwenye dini ya baba yake huku akibadili jina na sasa anaitwa Amina Sengo.

“Nimerudi kwenye dini ya baba yangu ambaye alikuwa Muislam na aliitwa jina la Juma Sengo.

 

Jina ambalo nilikuwa ninatumia la Wellu Juma Sengo, sasa nitakuwa natumia Amina Juma Sengo, nawaomba ndugu zangu wanishike mkono katika imani hii ingawa wengi wam enizodoa wakidai huenda nimepata mwanaume wa Kiislam ambaye anataka kunioa, lakini si kweli,” alisema Wellu ambaye hivi karibuni alitengana na Steve Nyerere.

STORI: IMELDA MTEMA,DAR

Comments are closed.