The House of Favourite Newspapers

Wengine wakitembea, Rayvanny anakimbia

0

KUNA usemi wa Kiswahili usemao kwamba kama unataka kuwahi kufika safarini, wakati wenzako wanatembea, wewe kimbia.

Hicho ndicho anachokifanya msanii Rayvann kwenye eneo la kuvuka mipaka na kwenda kimataifa zaidi.

Kupitia muziki wake na kolabo anazozifanya na wasanii kutoka mataifa hata yasiyotarajiwa, Rayvanny ameongeza tuzo baada ya kushinda Tuzo ya Hipipo Music Award katika Kipengele cha African Best Act 2021.

Tuzo hizo kutoka Uganda zimemtaja Rayvanny kushinda tuzo hiyo kupitia wimbo wa Mama Tetema ambao ameshirikishwa na mwanamuziki kutoka nchini Colombia aitwaye Maluma; wimbo huo ni Remix version ya wimbo wa Rayvanny wa Tetema.

STORI; SIFAEL PAUL, DAR

Leave A Reply