WOLPER; KIBOKO KWA KOPI & PASTE
HAKUNA kitu kizuri duniani kama kubarikiwa kuwa na kipaji ambacho unaweza kukifanya na jamii ikakukubali.
Jacqueline Wolper ni mmoja kati ya wasanii waliobarikiwa kuwa na vipaji, ukiachana na kuigiza ambapo ndipo kumempatia jina, Wolper ni bonge la mbunifu wa mavazi.
Ameshawavalisha mastaa wengi na pia amekuwa akibuni mavazi yake mwenyewe yanayotambulika kama ‘parachuti’.
Kuiga si dhambi, lakini kwa siku za hivi karibuni mavazi mengi ambayo Wolper amekuwa akionekana nayo ama kuwabunia watu basi yanakuwa ni kopi na pesti kutoka kwa mastaa wa Marekani akiwemo staa wa Muziki wa Pop, Rihanna.
Katika makala haya yanachambua baadhi ya mavazi hayo;
UZINDUZI WA NUMBER ONE
Katika uzinduzi wa video ya Wimbo wa Number One ya Diamond uliofanyika ndani ya Hoteli ya Serena, Wolper alitokelezea na gauni ambalo wiki hiyohiyo Rihana alikuwa amelitinga katika Tuzo za Grammy.
UZINDUZI WA CHANELI
Mbali na kupenda kukopi mavazi hayo ya Rihanna na kutokelezea, ishu nyingine ilikuwa katika uzinduzi wa chaneli ya kiswahili ya filamu inayopatikanika katika king’amuzi cha Dstv.
Katika usiku huo, Wolper alitokelezea na gauni kubwa jeusi la parachuti ambapo gauni kama hilo liliwahi kuvaliwa na Rihanna lakini utaofauti wake ukawa ni rangi kwani la Rihanna lilikuwa la ‘light blue’.
BIRTHDAY YA SWEET FELLA
Hii nayo iliongelewa sana mitandaoni baada ya Wolper kumbunia gauni jeupe mke wa Mkurugenzi wa Mkubwa na Wanawe, Said Fella aitwaye Sweet.
Sweet Fella alitinga gauni hilo siku yake ya kuzaliwa ambapo lilikuja kujulikana kuwa, Wolper alilipesti kutoka kwa Rihanna.
SHOO YA PAPII
Juzikati katika shoo ya kwanza kwa wanamuziki ndugu, Papii na Babu Seya iliyofanyika katika Ukumbi wa King Solomon, Wolper alitinga tena na gauni la kupesti.
Katika usiku huo, Wolper aliingia akiwa na parachuti la rangi ya ‘damu ya mzee’ ambalo ilibainika amelipesti kutoka kwa rapa wa kike, Cardi B.
NA IMELDA MTEMA.
Comments are closed.