Bethidei ya Jike Shupa Yavurugika, Polisi Wavamia
LEO ni siku ya kuzaliwa ya muuza sura kwenye video za wasanii wa Bongo Fleva, Zena Abdallah ‘Jike Shupa’ sherehe yake imevurugika kufanyika kutokana na Polisi kuvamia sherehe hiyo iliyikuwa inafanyika nyumbani kwake na kuwakamata vijana kadhaa wakidaiwa kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya maarufu kama Bangi.
Sherehe hiyo ilikuwa ifanyike usiku huu nyumbani kwake Mwananyamara jijini Dar lakini imeshindikana kutokana vurugu hizo zilizoibuka hatua iliyopelekea pia waandishi wetu waliokuwa eneo la tukio kushindwa kufanya kazi yao kwa ufanisi.
Marafiki wa Jike Shupa wakiwa kaika picha ya pamoja kabla ya sherehe hiyo kuanza.
(PICHA: DENIS MTIMA/GPL)