The House of Favourite Newspapers

Yanga dhidi ya Simba ‘Kariakoo Derby’ Kuchezwa Aprili 20, 2024

0

Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/2024 kati Yanga dhidi ya Simba Sc almaarufu ‘Kariakoo Derby’ ambao awali haukupangiwa tarehe kwenye ratiba iliyofanyiwa maboresho na kutangazwa Februari 2024, sasa utachezwa Aprili 20, 2024 kuanzia saa 11:00 jioni katika dimba la Benjamin Mkapa.

Taarifa ya bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imebainisha kuwa Yanga na na Simba pamoja na wadau wengine wa Ligi Kuu ya NBC wamepatiwa taarifa zote kuhusiana na mchezo huo na maandalizi yake yanaanza mara moja ili kuhakikisha unafanyika katika kiwango cha juu kinachoendana na hadhi ya michezo mikubwa ya Ligi ya sita kwa ubora barani Afrika.

Leave A Reply