Yanga Waanza Kujifua Kuelekea Msimu Mpya
Wachezaji wa Timu ya Yanga wameanza kujifua mazoezi kwenye Uwanja wa Chuo cha Sheria jijini Dar es Salaam kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Jana, Jumatatu, Agosti 10, 2020 wachezaji 11 walifika Uwanjani hapo na kuanza kupiga mazoezi kujiandaa na msimu mpya.
Miongozi mwa wachezaji hao wamo wapya na waliokuwepo klabuni hapo.