The House of Favourite Newspapers

Yanga yasaka straika wa kazi

0

AmissTambwe2.jpgAmissi Tambwe.

Na Wilbert Molandi
YANGA ina washambuliaji watatu wa kutegemewa ambao ni Donald Ngoma, Amissi Tambwe na Malimi Busungu, lakini bado haijatosheka, uongozi wa timu hiyo upo kwenye mipango ya kusajili straika mwingine wa kazi.
Awali, mabingwa hao wa Ligi Kuu Bara, walitangaza kwamba hawatasajili mchezaji yeyote wakati huu wa dirisha dogo lakini wametengua kauli yao, baada ya kuona jinsi wapinzani wao Simba wanavyojiimarisha.

Straika huyo amepangwa kusajiliwa kwenye usajili wa dirisha dogo msimu huu kwa ajili ya kuichezea timu hiyo kwenye Ligi Kuu Bara na Ligi ya Mabingwa Afrika, mwakani.
Yanga inataka kusajili straika mwingine baada ya kocha mkuu wa timu hiyo, Hans van Der Pluijm kupendekeza kutokana na Busungu kuhamishiwa pembeni namba 11 iliyokuwa inachezwa na Andrey Coutinho na Geofrey Mwashiuya.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Katibu Mkuu wa timu hiyo, Dk Jonas Tiboroha, alisema kuwa mshambuliaji wanayemtaka ni yule aliye tayari kwa ajili ya kucheza ligi kuu na michuano mingine.
Tiboroha alisema, straika huyo wanayemtaka ni yule atakayefanya mazoezi na timu siku mbili na siku inayofuata anaingia uwanjani kwa ajili ya kufanya kazi na siyo vingine.
Aliongeza kuwa, huo ndiyo mfumo wa usajili watakaoutumia katika usajili wa wachezaji wao kimataifa

katika kuhakikisha timu yao inakwenda kisasa.
“Yapo mapendekezo mengi ya usajili yaliyotolewa kutoka katika benchi letu la ufundi, moja kati ya nafasi tunayoitazama hivi sasa ni safu ya ushambuliaji ambayo lazima tusajili.

“Hivyo kama usajili huo tutaufanya, basi lazima tumsajili straika wa kazi mwenye uwezo wa kufunga mabao na aliye tayari kwa ajili ya kufanya kazi na siyo kumfanyisha majaribio.
“Straika huyo tutakayemsajili ni yule atakayeendana na kasi kwa maana ya kufanya mazoezi kwa siku mbili na kesho yake akaingia uwanjani kufanya kazi kwa kucheza mechi na siyo kutoa muda wa majaribio,” alisema Tiboroha.

Leave A Reply