The House of Favourite Newspapers

YANGA YASHIKWA SHATI NA LIPULI ZATOKA 1-1

0
Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma akimtoka beki wa Lipuli.

 

FULL TIME

Dakika ya 94: Mchezo umemalizika kwa matokeo ya bao 1-1.

Dakika ya 93: Kwasi wa Lipuli anapewa kadi ya pili ya njano, anatoka huku akilalamika.

Dakika ya 90: Mwamuzi wa kwenye benchi anaonyesha dakika 4 za nyongeza, kuna mchezaji wa Lipuli yupo chini.

Dakika ya 90: Mashabiki wa Yanga wanaonekana kukata tamaa. Mchezo bado unaendelea.

Polisi wakiwadhibiti mashabiki wa Yanga na Lipuli.

Dakika ya 88: Bado mambo magumu kwa timu zote.

Dakika ya 84: Tshishimbi anapewa kadi ya njano kwa kucheza faulo, analalamika lakini mwamuzi anapa kadi hiyo.

Dakika ya 79: Lipuli wanarudi nyuma, muda mwingi mpira unachezwa kwenye nusu yao.

Dakika ya 78: Yanga wanafanya mashambulizi lakini bado mambo magumu.

Dakika ya 70: Yusuph Mhilu wa Yanga anaingiam anatoka Emmanuel Martine.

Mchezaji wa Lipuli (kushoto) akimtati Donald Ngoma.

Dakika ya 69: Mchezo unaendelea, wachezaji wa timu zote wanatumia nguvu kubwa kupambana.

Dakika ya 65: Tshishimbi anachezewa faulo mguuni, mchezo unasimama anatabiwa.

Dakika ya 60: Mchezo ni mgumu kwa timu zote

Dakika ya 55: Lipuli wanajibu mapigo kwa kulishambulia lango la Yanga kila wanaposhambuliwa.

Dakika ya 49: Yanga wanacheza kwa kasi lakini upinzani ni mkali.

Kipindi cha pili kimeanza.

…Donald Ngoma akiwatoka wachezaji wa Lipuli.

Mapumziko

Dakika ya 47: Wachezaji wa Lipuli wanalalamika kuwa mpira ulikuwa haijaingia baada ya Ngoma kuupiga kichwa, lakini mwamuzi anaweka kati.

Dakika ya 45: GOOOOOOOOOOOOOOO!!! Yanga wanasawazisha kupitia kwa Ndoma lakini utata unatokea.

Lipuli wanapata bao kupitia kwa Seif Abdallah ambaye akicheza vizuri kwa kuwatoka walinzi wa Yanga kabla ya kufunga.

Dakika ya 44: GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO!!!

Dakika ya 42: Matokeo bado ni 0-0, timu zote hazijafanya mashambulizi makali mengi.

Dakika ya 39: Mpira unachezwa zaidi katikati ya uwanja.

Dakika ya 36: Kipa wa Lipuli anachezewa faulo wakati wa kona, mchezo unasimama kwa dakika mbili kisha unaendelea.

Dakika ya 33: Mchezo unaendelea kwa kasi.

Dakika ya 28: Yanga wanafanya shambulizi kali lakini linakuwa halina faida.

Dakika ya 24: Lipuli wanaonyesha kujiamini na kuwabana Yanga.

Dakika ya 22: Yanga wanapata kona lakini haina faida.

Dakika ya 21: Lipuli wanaonyesha kuwa na makali, wanalishambulia lango la Yanga, almanusura wapate bao lakini mpira wa kichwa unapaa juu ya lango.

Dakika ya 18: Yanga wanaanza kupanga mashambulizi licha ya upinzani mkali kutoka kwa Lipuli inayofundishwa na Selemani Matola.

Dakika ya 11: Yanga wameshacheza faulo mara mbili, Lipuli mara 4.

Dakika ya 5: Yanga wanamiliki mpira muda mwingi.

Dakika ya 2: Mchezo umeanza kwa kasi ndogo.

Kipindi cha kwanza kimeanza, huu ni mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, timu zote zimeingia uwanjani kucheza mchezo wao wa kwanza msimu wa 2017/18.

PICHA: RICHARD BUKOS/GPL

Leave A Reply