Isabela Amfagilia Gwajima
UFAGIO! Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, Isabela Mpanda amemfagilia Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima kwa jinsi anavyojiamini kiasi kwamba yupo tayari kuhudhuria ibada zake.
Akizungumza na Za Motomoto News, Isabela alisema anatamani kuwa karibu na mchungaji huyo kwani anayejiamini, anahubiri na kutoa mafundisho kwa waumini wake bila hofu hivyo anatarajia kuanza kwenda kuhudhuria ibada anazoziendesha kanisani kwake kila wakati.
“Nampa big up sana Gwajima maana anajiamini hivyo nitaanza kwenda kanisani kwake ili kuhudhuria ibada zake kwa lengo na kujifunza mengi,” alisema
Comments are closed.