The House of Favourite Newspapers

Skendo Zampa Stress Davido, Alazwa Hospitali!

David Adeleke ‘Davido’.

Na MWANDISHI WETU| GAZETI LA IJUMAA| KUTOKA NAIJAS

MKURUGENZI wa Lebo ya HKN, David Adeleke ‘Davido’ amekimbizwa hospitali na kulazwa huku chanzo kikidaiwa kuwa ni ‘stress’. Tukio hilo limejiri juzikati ambapo inaelezwa kuwa, Davido amekuwa akisumbuliwa na skendo inayozidi kuenea kwa kasi kuhusiana na kuzaa na mwanamke anayefahamika kama Ayomide Labinjo.

Davido na mwanaye.

Haikuelezwa hasa hospitali ipi amelazwa lakini kupitia Mtandao wa Snaptchat, Davido liweka kipande cha video akiwa ametundukiwa dripu na kuwaambia mashabiki wake wamuombee.

Hivi karibuni, Ayomide alizungumza na Jarida la Punch na kuanika kila kitu kuwa, amezaa na Davido baada ya kulazimishwa wasitumie kinga.

“Kama Davido unanisikiliza ulijue hili kuwa uligoma kutumia kinga,” Ayomide aliliambia Punch. Tayari, Ayomide kwa kushirikiana na mama yake wameshafungua mashtaka yakumtaka Davido ashiriki katika malezi ya mtoto huyo.

 

Comments are closed.