The House of Favourite Newspapers

Aunty Lulu Sasa Kuimba Gospo

0
Lulu Semagongo, ‘Aunty Lulu’.

  Na MWANDISHI WETU/GPL

BAADA ya maisha ya ujana yenye kila aina ya uchafu hatimaye msanii na Mtangazaji Lulu Semagongo maarufu kama Aunty Lulu, amesema anajiandaa kuimba nyimbo za Injili zitakazozungumzia maisha yake ili watu wengine wajifunze.

Aunty Lulu alisema nyimbo zake zitabadilisha maisha ya watu wengi kwani ujumbe utakaokuwemo ndani yake utazungumzia mambo mengi ambayo amepitia katika maisha yake.

Aunty Lulu akiwa na rafiki yake.

“Najiandaa kuimba nyimbo za Injili na wimbo wangu wa kwanza utaitwa Unikumbuke Mungu, ambapo ndani yake nitaeleza mambo yote niliyopitia kwenye maisha yangu ikiwemo kubadilisha wanaume tofauti, starehe za kila aina, kuvuta sigara na mengine mengi na nimeamua kufanya hivi ili kupitia historia ya maisha yangu vijana wengi wabadilike,” alisema.

 

Leave A Reply