The House of Favourite Newspapers

‘Matepeli’ Wavamia Wageni Uwanja wa Oliver Tambo ‘Sauzi’

0
Uwanja wa ndege wa O. R. Tambo Afrika Kusini.

Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imetoa tahadhari kwa Watanzania wanaoingia Afrika Kusini kupitia Uwanja wa Ndege wa Oliver Tambo, ambapo kuna magenge ya watu wanaoendesha vitendo vya kuvamia na kunyang’anya wageni kutoka nchi mbalimbali mali zao zikiwemo fedha taslim, mabegi, nguo , pete za ndoa na vitu vingine vya thamani.

Uporaji huu hutokea hasa kwa wasafiri wanaoingia nchini humo kuanzia saa 12 jioni na kuendelea.  Mbinu zinazotumika kuwatapeli na kuwaibia wageni zipo chini katika barua iliyotolewa na wizara hiyo.

Leave A Reply