Chai ya nyanya kwa kutibu mafua
Wiki hii tunakuja na tiba ya mafua sugu ambayo ukiitumia ndani ya siku tatu unapona kabisa, hii si nyingine bali ni chai ya nyanya ambayo inachanganywa na kitunguu swaumu na limao.
Jinsi unavyoichanganya na kupata chai
Chukua kikombe cha juisi ya nyanya, changanya na kitunguu swaumu kilichosagwa, kisha weka kijiko cha chai cha limao.
Baada ya hapo weka kwenye moto ichemke kama chai kisha unywe ikiwa ya moto hivyohivyo.
Faida ya tiba hii
Juisi ya nyanya ina vitamin C nyingi ambayo inasaidia kuimarisha kinga ya mwili, kitunguu swaumu kinasaidia kuondoa maambukizi.