Albam ya P Funk Imekamilika, Soon Inaingia Sokoni
HATIMAYE mtayarishaji nguli wa muziki wa Bongo Fleva, Paul Matthysse maarufu kama P Funk Majani, ametangaza rasmi ujio wa albam yake mpya itakayoitwa jina lake maarufu la kazi ‘Majani’.
P Funk kupitia ukurasa wake wa Twitter ameposti ujumbe wenye taarifa kwa ufupi kuhusu ujio wa albam hiyo;
“Album yangu ‘#MAJANI‘ imekamilika kwa takribani asilimia 80, mwenyezi Mungu akipenda nitaiachia Machi 30, 2022,” ameandika P Funk.