The House of Favourite Newspapers

Aliyezawadiwa Kitabu cha Shigongo Afunguka

0

MWANDISHI mahiri wa vitabu Afrika Mashariki na Kati, Eric Shigongo, kupitia magazeti bora ya michezo ya Spoti Xtra na Championi, anatoa zawadi za vitabu kwa wasomaji wa magazeti hayo.

 

Miongoni mwa waliozawadiwa vitabu hivyo ni Richard Mbano, ambapo ameelezea furaha yake baada ya kupokea zawadi hiyo mapema leo Ijumaa kwenye ofisi za Global Publishers zilizopo Sinza Mori, Dar.

Kupitia Gazeti la Championi linalouzwa kwa Sh 800 na kupatikana mtaani kila siku za Jumatatu, Jumatano, Ijumaa na Jumamosi sambamba na Spoti Xtra linalouzwa Sh 500 na kuingia mtaani Jumanne, Alhamisi na Jumapili, msomaji anapata fursa ya kutunukiwa zawadi ya vitabu kama Rais Anampenda Mke Wangu, Kifo ni Haki Yangu, Machozi na Damu na vitabu vya ujasiriamali.

 

Kwa maelezo zaidi namna ya kupata zawadi za vitabu hivyo, soma magazeti ya Spoti Xtra na Championi.

Leave A Reply