The House of Favourite Newspapers

Azam FC Hawajakata Tamaa Ligi Kuu

0

VIVIER Bahati, kocha msaidizi wa Azam FC amesema kuwa bado hawajakata tamaa licha ya kupata sare ya bila kufungana mbele ya Mwadui FC.

 

 

 

Kwenye mchezo wao wa ligi uliochezwa Uwanja wa Mwadui Complex, ubao ulisoma Mwadui FC 0-0 Azam FC na kuzifanya timu hizo kugawana pointi moja-moja.

 

 

 

Matokeo hayo yanaifanya Azam FC kufikisha jumla ya pointi 41 ikiwa imecheza jumla ya mechi 23 na Mwadui ipo nafasi ya 18 ikiwa na pointi 23 baada ya kucheza mechi 23.

 

 

 

Kinara wa ligi ni Yanga mwenye jumla ya pointi 50 akiwa amecheza jumla ya mechi 23 ndani ya ligi, msimu wa 2020/21.

 

 

 

Vivier amesema: “Bado tuna nafasi ya kufanya vizuri na kupata matokeo chanya kwenye mechi zetu zijazo kwa kuwa vijana wana morali kubwa na uwezo wao unazidi kuwa vizuri kila leo.

 

 

 

“Kugawana pointi moja kwenye mechi yetu iliyopita haina maana kwamba ni mwisho wa mashindano bado tuna nafasi ya kuendelea kufanya vizuri hivyo mashabiki watupe sapoti na tutafanya vizuri.”

Leave A Reply