The House of Favourite Newspapers

Baada ya Kudaiwa Kuachana na Simba, ‘Mo’ Atoa Ujumbe Mzito

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Klabu ya Simba, ambaye pia ni mwekezaji wa timu hiyo, Mohammed Dewji ‘Mo’ amejibu kuhusu taarifa zilizosambaa mitandaoni zikidai kuwa wakati wowote kuanzia sasa atajiondoa katika klabu hiyo.

 

Taarifa hizo zilizoanza kusambaa jana usiku katika mitandao ya kijamii, lakini mwenyewe amejitokeza na kuweka bayana kinachoendelea.

 

Kupitia ukurasa wake wa Twitter pamoja na Instagram, Mo ameandika ujumbe mzito ambao umekuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii na kuacha maswali mengi. Ameandika: “Watu wenye nia mbaya, kazi yao ni kuvunja tu. Kaa nao mbali, narudia kaa nao mbali sana!

TAZAMA VIDEO HII

Comments are closed.