Ben Pol Abadili Dini, Awa Muislam
MSANII maarufu wa miondoko ya RnB nchini, Ben Pol, jana Ijumaa, Oktoba 23, 2020 ametangaza kubadili itikadi ya dini kitoka Ukristo na kuwa Muislamu.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, mkali huyo wa Bongo Fleva ameposti picha zilizoambatana na nakala ya cheti cha kubadilisha dini.
Awali Ben Pol alikuwa akitumia jina la Bernard Paul na sasa anatambulika kama Behnam.