The House of Favourite Newspapers

Bernard Morrison Amuwakia Manara

0

KIUNGO Mshambuliaji wa Simba Mghana, Bernard Morrison amemjia juu msemaji wa klabu ya Yanga, Haji Manara akimsihi awe na busara dhidi ya kauli tata ambazo amekuwa akizisema dhidi ya klabu yake ya zamani.

 

Uongozi wa klabu ya Simba Julai 28, mwaka huu ulitangaza rasmi kuondoka kwa Haji Manara na kumtangaza Ezekiel Kamwaga kuwa kaimu Ofisa habari mpya wa klabu hiyo.

 

Tangu ameondoka Simba, Manara mara kwa mara ametoka hadharani na hata kupitia mindao yake ya kijamii amekuwa akitoa kauli tata dhidi ya baadhi ya viongozi wa juu wa timu hiyo hususani Ofisa Mtendaji Mkuu, Barbara Gonzalez na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa timu hiyo, Mohammed Dewji ‘MO’Kufuatia posti ya Msemaji wa Yanga, Haji Manara aliyoiweka jana Jumanne katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram ya kumsifia bosi na mdhamini wa klabu hiyo, Ghalib Said Mohammed ‘GSM’, na kuonyesha maneno ya kejeli kwa yule aliyemuita bosi wa Instagram.

Morrison alimjibu kwa kuandika: “Niliondoka Yanga bila kuwa na maelewano mazuri nao, na mpaka sasa bado hatuna mahusiano mazuri, lakini sikuwahi kuzungumza chochote kibaya kuihusu klabu wala kumhusu Injinia Hersi Said, wala Antonio Nugaz wala mashabiki wao, unajua kwa nini?

 

“Hii ni kwa sababu walinitunza na kunifanyia mema mara nyingi, hivyo siwezi kuwavunjia heshima licha ya kwamba kuna matatizo kati yetu. Hiyo ndiyo busara kaka.

 

Usiung’ate mkono ambao unakulisha, au uliowahi kukulisha.“Kuna msemo usemao busara ni kawaida isipokuwa tu kwa watu wa kawaida, huu ni ushauri tu kwako kaka mkubwa, ukweli unauma lakini hakuna hisia isiyovumilika.”

STORI: JOEL THOMAS,Dar es Salaam

Leave A Reply