The House of Favourite Newspapers

Breaking: Dkt. Tulia Ndiye Mshindi wa Uspika

0

Mbunge wa Mbeya Mjini, Dk. Tulia Ackson amechaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupata kura zote 376 za wabunge katika Uchaguzi uliofanyika leo Jumanne Februari 1, 2022 bungeni jijini Dodoma.

Akitangaza matokeo hayo, Mwenyekiti wa Uchaguzi huo, William Lukuvi amesema Mhe. Dkt. Tulia amewashinda wagombea wengine nane ambao wote wamepata kura 0 na hakuna kura iliyoharibika.

Leave A Reply