Jinsi ya kupika Maboga ya Nazi
Nakukaribisha mpenzi msomaji wangu katika safu hii ya Mahanjumati ambapo kutokana na meseji zenu leo tutajifunza kupika maboga ya nazi. Chakula ambacho ni rahisi sana kupika.
MAHITAJI
Boga moja
Nazi moja
Sukari kiasi unachotaka
Hiliki nusu kijiko
KUANDAA NA KUPIKA
Kuna nazi kisha chuja tui vikombe viwili weka pembeni.
Menya maboga kiasi ukipendacho.
Yakate vipande vidogovidogo.
Washa jiko kisha bandika maboga yaache mpaka yaive lakini humwagi maji na hakikisha hayavurugiki.
Maji yakishaanza kukauka weka sukari kiasi ukipendacho na hiliki.
Mimina tui la nazi na uliache lichemke na kuiva vizuri.
Likishachemkia vizuri na kubaki na supu kiasi epua na chakula chako (maboga) kitakuwa tayari kwa kula.