Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amesimama na kuwasalimia wafanyabiashara wa mazao eneo la Dumila, Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro na kuwaahidi kuwapatia shilingi Milioni mia moja kwa ajili ya Ujenzi wa mabanda ya kisasa.
Magufuli ametoa ahadi hiyo baada ya wafanyabiashara hao kumuomba waongezewe eneo hilo lililopo kando ya Barabara iendayo Dodoma.
Aidha, Rais Magufuli amenunua muhindi kwa vijana wachoma mahindi wa eneo hilo la Dumila aliposimama kuwasalimia wafanyabiashara hao.