Justin Bieber apata ‘kifaa’ kipya!
STAA wa muziki nchini Marekani asiyeishiwa vituko, Justin Bieber baada ya kuachana na mpenzi wake Kourtney Kardashian amepata mpenzi mpya aitwaye Alexandra Rodríguez na wameonekana pamoja wakijivinjari kwenye fukwe za Miami huko Florida.
Mrembo huyo mpya anafanana sana na mpenzi wa zamani wa Beiber, Selena Gomez. Vyombo mbalimbali vimekuwa vikiripoti uhusiano huo wa kimapenzi baina ya Beiber na Alexandra Rodríguez hakuna hata mmoja aliyethibitisha kuwa wana uhusiano wa kimapenzi.
Picha kibao zilizopigwa wakati wakiwa ufukweni zimeanza kuwaaminisha mashabiki wao wengi kuwa ni kweli wana uhusiano wa kimapenzi kutokana na ukaribu wao.