Kisa sms… Lindsay, baby wake wazinguana kinoma shereheni
Muigizaji Lindsay Lohan juzikati alijikuta akidata baada ya kuona ujumbe wa kimapenzi kutoka kwa mwanamke mwingine kwenye simu ya mpenzi wake aitwaye Egor Tarabasov, hali iliyoibua ugomvi.
Wawili hao walikuwa wamekwenda kwenye Kisiwa cha Mykonos kulikokuwa na sherehe lakini ghafla furaha yao ikaingiwa na mdudu.
Inaelezwa kuwa, wakati wapenzi hao wakiendelea kula bata huku mama wa Egor akiwa karibu yao, Lindsay aliona sms ambayo haikumfurahisha, kwa hasira aliichukua simu ya mpenzi wake na kuitupa baharini.
Kitendo hicho kilimfanya Egor kumkunja na kummwagia Lindsay kinywaji, hali iliyomfanya mama wa Egor kusikitika na kuondoka huku Lindsay naye akienda kupanda gari na kuondoka zake.
Baadaye Lindsay aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kuwa mapenzi yanaua hasa ukiwa mtu mzima na ukapitia mazito.