The House of Favourite Newspapers

Kukosa mtoto kwamtesa Lulu Diva

0

 

MSANII wa Bongo Fleva na Bongo Movies, Lulu Abbas au Lulu Diva anasema kuwa suala la kukosa mtoto linamtesa na kwamba anamuomba Mungu amjalie uzao wake na yeye.

 

Lulu Diva anasema kuwa, kwa sasa hana mtoto ila anatamani mno siku moja aitwe mama kama walivyo wamama wengine kwani huko ndiko kuwa mwanamke kamili.

 

“Kwa sasa sina mtoto hata wa dawa ila kiukweli natamani sana kuitwa na mimi mama Mungu anijaalie juu ya hilo,” anasema Lulu Diva ambaye amekuwa akimficha mpenzi wake.

STORI; KHADIJA BAKARI, DAR

Leave A Reply