Rais Samia Awasili Nchini “Dunia Inawasalimia” – Video
“Tumekwenda kwenye safari ambayo kwa miaka 6 tumekuwa tukiwakilishwa na ngazi ya Uwaziri na Ubalozi, lakini hatukwenda kama kiongozi wa nchi, mara hii tumekwenda, tumeshiriki na wenzetu na dunia inawasalimia.
“Katika mkutano ule tulikuwa na mambo manne makubwa, moja ni masuala ya uchumi na namna yalivyoathiriwa na maradhi ya UVIKO-19. Pili ni masuala yote ya UVIKO-19, kuhusu chanjo na kushirikiana jinsi ya kushinda janga hili.
“La tatu ni masuala ya utawala bora katika nchi zetu na utawala bora duniani. Pia tuligusia kuhusu masuala ya mazingira, kwa niaba ya Watanzania iliiahidi dunia kwamba Tanzania tutayafanyia kazi yote haya ili twende na dunia inavyokwenda.
“Nimepata fursa ya kuonana na Rais wa Benki ya Dunia, Rais wa Baraza la Umoja wa Ulaya, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Biashara Duniani, wafanyabiashara wa marekani waliowekeza Tanzania na wanaotaka kuja Tanzania, nimeonana na Marais wenzangu, orodha ni kubwa.