JPM: “Wananchi Wanakufa, Aliyechoma Mradi wa Maji Akamtwe Sasa Hivi” – Video
Rais Dk. John Magufuli leo Jumapili Oktoba 6, 2019 ameanza ziara ya siku tatu mkoani Rukwa ambapo anatarajiwa kufungua barabara ya Tunduma – Sumbawanga yenye urefu wa Kilomita 223.21. Rais Magufuli yupo katika ziara ya siku tisa katika mikoa ya Songwe, Rukwa na Katavi.
Magufuli amesema ameanza ziara yake ya kikazi mkoani Rukwa kwa majonzi baada ya kuona fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi hazifanyi kazi iliyokusudiwa;
“Mbunge huyu alikuwa akinisumbua tangu nikiwa waziri, Daraja la Momba alinisumbua kweli, anapenda jimbo lake. Lakini binadamu ukiafanyia kazi atakusema vibaya, unamvusha kwenye mto anakwambia mgongo wako unanuka, una jasho. Ilikuwa aitwe kwenye kamati ya CCM afukuzwe, lakini alikuwa imara kuwatetea wananchi wake na leo matunda yanaonekana.
Comments are closed.