Maalim Azungumzia Corona, Madeni Nchi Changa Yasimamishwe – Video
MWENYEKITI wa ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharrif Hamad, leo Aprili 4, 2020, ametoa rai kwa Watanzania kuchukua tahadhari zote dhidi ya ugonjwa wa Covid-19 unaoambukizwa na virusi vya Corona, na amezitaka nchi zilizoendelea kusimamisha kwa mwaka mmoja madeni dhidi ya nchi zinazoendelea ili kuzipa nchi hizo nafasi ya kujenga mfumo bora wa huduma za afya
Ameyasema hayo katika mkutano na waandishi wa habari katika ofisi za chama hicho huko Zanzibar ambapo amewataka wakazi wa visiwa hivyo kuwa walinzi dhidi ya watu kutoka nje ili kuzuia maambukizo ya virusi hivyo hatari.