The House of Favourite Newspapers

Madai Nisha amfuata Bwanake’ke Tatuu ya Shilole

0
Mwigizaji mwenzake, Zuwena Mohammed ‘Shilole’.

UBUYU wa mahaba niue! Ndiyo maneno unayoweza kusema baada ya staa wa filamu za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ kudaiwa kumfuta tatuu (mchoro wa mwilini) bwana’ke mpya aitwaye Boy Caro iliyokuwa na jina la mwigizaji mwenzake, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ ambaye ndiye mtangulizi aliyekuwa anaminya na jamaa huyo kabla ya kumwagana.

Awali, Boy Caro alikuwa na uhusiano wa wazi wa kimapenzi na Shilole huku wakioneshana mapenzi ya njiwa na kujikuta akichora tatuu ya jina la ‘Shishi Baby’ kwenye ubavu wake ambayo kwa sasa inadaiwa kufutwa na ‘mmiliki’ mpya ambaye ni Nisha.

Staa wa filamu za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’.

TUJIUNGE NA CHANZO

Chanzo ambacho kiko karibu na wawili hao kililimwagia Wikienda ubuyu kuwa, kutokana na mapenzi ‘shatashata’ yaliyopo kati ya Boy Caro na Nisha, mwanamama huyo amemfuta tatuu hiyo kwa kile kilichodaiwa kuwa ilikuwa ikimchefua na kuwa kero kubwa kwake.

“Yaani Nisha hataki mchezo kabisa maana kwa jinsi anavyopendana na Boy Caro, ameamua kumfuta na tatuu aliyokuwa nayo ya Shishi Baby kwa sababu walishaachana na sasa yuko naye hivyo akawa anaiona kama kero kwake na kwamba inaweza ikamrudisha jamaa kwa Shilole hivyo dawa yake ni kuifuta tu.

“Siku chache tu zilizopita walikuwa uwanja wa ndege (Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar) pamoja ambapo Boy Caro alimsindikiza Nisha ambaye ameenda nchini China kuchukua mzigo wa dukani.

“Yaani walikuwa wanaoneshana mahaba niteketeze utadhani ndiyo wameshahalalishwa kuwa mke na mume kabisa. Duh! Ungewaona ungeamini mapenzi ya awali matamu lakini ya mwishoni huwa ni shubiri. Walionekana wapo kwenye sayari yao.

“Baada ya kuhakikisha Nisha amepanda ndege, Boy Caro alirudi wanapoishi maeneo ya Mikocheni (Dar) akiwa na gari la mpenzi wake huyo bila kuwa na wasiwasi wowote,” kilifunguka ‘kikulacho’ hicho.

WIKIENDA LAMSAKA NISHA

Baada ya kupata ubuyu huo, Wikienda lilimsaka Nisha kwa njia ya simu lakini hakupatikana na alipotafutwa kwa njia ya Mtandao wa Kijamii wa WhatsApp ilikuwa hivi;

Wikienda: Mambo vipi Nisha?

Nisha: Poa, leta ubuyu maana nawajua ninyi mkinitafuta kuna kitu.

Wikienda: Ni kweli kuna kitu. Kuna habari kwamba umemfuta tatuu bwana’ko, Boy Caro iliyokuwa na jina la Shishi Baby maana ilikuwa inakukera, hii ishu ikoje?

Nisha: Jamani kufuta au kuchora tatuu ni mapenzi ya mtu.

Wikienda: Lakini inasemekana wewe ndiye uliyemtaka aifute kwa lazima!

Nisha: Sijamfuta mtu tatuu kwani naamini mapenzi yapo moyoni. Unaweza kumfuta kwenye ngozi ila moyoni ukashindwa, halafu kama mtu ameamua kufuta ni mapenzi yake, isihusishwe na mimi maana siamini mapenzi ya kuchorana tatuu bali namuomba Mungu mpenzi wangu anichore moyoni.

Wikienda: Hivi karibuni umeonekana uwanja wa ndege ukiwa na Boy Caro ambaye alikusindikiza wakati unaondoka Bongo kwenda China, je, ni kweli?

Nisha: Kweli niko China, alinisindikiza kama rafiki tu jamani.

NENO LA MHARIRI

Kama ulikuwa hujui, huo ndiyo ubuyu wa mjini lakini bado Nisha analalamikiwa kwa kitendo cha kumchukua mwanaume ambaye alishajua ametembea na mwigizaji mwenzake hivyo alitakiwa kumkwepa kwa sababu kumekuwa na maneno mengi juu ya tabia ya mastaa wa Bongo Muvi kupokezana mabwana.

Stori: Gladness Mallya, Wikienda

Leave A Reply