The House of Favourite Newspapers

Majibu ya Esma Kuhusu Diamond Kumuoa Zuchu

0

BAADA ya kuwepo kwa tetesi nyingi mitandaoni juu ya staa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz kuwa mbioni kumuoa Zuchu, dada wa jamaa huyo, Esma Platnumz ametoa majibu ya kile anachokijua.

Kama dada, Esma ameulizwa na mmoja wa wafuasi wake kwenye Instagram; je, ni kweli kaka yako anamuoa Zuchu?

Katika majibu yake, Esma akajibu; “Ahaa jamani…hii taarifa ndiyo kwanza ninaisikia kutoka kwako…”

Kwa mujibu wa Esma hicho kitu hakipo pamoja na kwamba kumekuwa na madai ya Diamond na Zuchu kutoka kimapenzi tangu aliposainiwa kwenye Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB).

Leave A Reply