The House of Favourite Newspapers

Mariah Carey Afunguliwa Kesi na Kaka Yake

0

MWANAMUZIKI wa miondoko ya Rnb Mariah Carey, amemfunguliwa kesi na kaka yake mkubwa kwenye mahakama kuu ya New York nchini Marekani akidaiwa kumdhalilisha kaka yake kwenye kitabu chake kinachofahamika kama The Meaning of Mariah Carey.

 

Kaka wa msanii huyo anataka alipwe dola milioni 1.25 sawa na Bil. 2 za Tanzania akimshtaki dada yake huyo kwa kumkashifu na kumsababisha matatizo ya akili kutokana na kumbukumbu yake alioandika kwenye kitabu chake.

 

Morgan Carey, ambaye anataka kulipwa kwa kuchafuliwa jina anasema kwamba kitabu hicho kinadai kwamba yeye anapenda vurugu.

 

”Kutokana na hilo amepata matatizo ya kiakili na kumuharibia sifa”, wamesema mawakili wake.

 

Leave A Reply