MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo, jana amewapongeza walimu, waratibu elimu na maofisa elimu wa Manispaa ya Kinondoni kwa matokeo mazuri ya darasa la saba mwaka jana na kushika nafasi ya tatu kitaifa.
Chongolo alitoa pongezi hizo jana kwenye hafla iliyofanyika Ukumbi wa Police Officers Mess, Oyster Bay jijini Dar.
Katika hafla hiyo shule zilizofanya vizuri zaidi zilitunukiwa vyeti na pesa taslimu katika kuwapa moyo wa kuendelea kufanya vizuri zaidi.
Mkuu huyo wa wilaya aliwapongeza walimu na wadau wote kwa kufanya kazi nzuri pamoja na wakati mwingine kukumbana na mazingira magumu ya kikazi.
HABARI: NEEMA ADRIAN
PICHA: RICHARD BUKOS /GPL