Membe Achukua Fomu Kuwania Urais
WAZIRI mstaafu wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, leo mchana Ijumaa, Julai 17, 2020, amechukua fomu ya kugombea urais kupitia chama cha ACT-WAZALENDO ikiwa ni siku moja tu baada ya kupokewa rasmi kwenye hicho.
Amechukua fomu hiyo katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Magomeni jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku moja baada ya uongozi wa chama hicho kumuomba agombee urais kupitia chama chao.