The House of Favourite Newspapers

Mke wa Bilionea Namba 1 Duniani Aolewa na Mwalimu

0

BILIONEA MacKenzie Scott, mtalaka wa mwanzilishi wa Amazon Jeff Bezoz ameolewa na mwalimu wa sayansi katika shule ya watoto wake.

 

 

Bi Scott ni mmoja wa wanawake tajiri zaidi duniani na ametoa zaidi ya dola bilioni nne ya mali yake. Taarifa ya kuolewa kwake na Dan Jewett ilifichuliwa kupitia tovuti ya kutoa misaada.

 

 

‘’Dan ni mtu mzuri, nawatakia kila la heri,’’ Bwana Bezos alisema katika taarifa. Bi Scott, ambaye thamani ya utajiri wake ni karibu dola bilioni 53 kulingana na makadirio ya hivi karibuni ya Forbes, amesema nia yake ni kutoa sehemu kubwa ya mali hiyo.

 

Leave A Reply