Mnaigeria Kuipa Shavu Bongo Muvi
MSANII wa Filamu kutoka Nigeria, Mike Ezuruonye, ‘Mikezuu’ jana alipokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ziara ya kikazi.
Mike amefunguka kuwa yupo nchini kikazi kuimalizia moja ya filamu aliyoshirikiana na wasanii wa hapa Bongo. Akipokelewa na mastaa wa filamu kibao wakiongozwa na Halima Yahya, ‘Davina’
“Nimefurahi sana kumuona Mike nchini Tanzania, karibu sana Mike pia mheshimiwa waziri samahani huwa tunatumia jina lako wakati wa kuomba vibali. Kazi hii ni kubwa na tunafanya hivi ili kuipanua soko la filamu nchini,” alisema Davina
Aidha Waziri wa Sanaa na Michezo Nape Nauye, alikuwepo uwanjani hapo.
Comments are closed.